Papa amemtua padre françois abeli muhoya mutchapa kuwa askofu wa kindu - | vatican news

feature-image

Play all audios:

Loading...

Papa Francisko amemteua Askofu wa Jimbo la Kindu katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC)Mhesh.Padre François Abeli Muhoya Mutchapa,padre wa Jimbo la Kindu,ambaye hadi uteuzi wake


alikuwa katika huduma ya kichungaji ya Parokia ya Mtakatifu Maria na Mtakatifu Mauro Jimbo la Tivoli(Italia). NA SR. ANGELA RWEZAULA – VATICAN. Papa Francisko amemteua Askofu wa Jimbo la


Kindu katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC) Mhesh. Padre François Abeli Muhoya Mutchapa, Padre wa Jimbo la Kindu, ambaye hadi uteuzi wakw alikuwa katika huduma ya kichungaji ya


Parokia ya Mtakatifu Maria na Mauro Jimbo la Tivoli (Italia). Askofu Mteule François Abeli Muhoya Mutchapa, alizaliwa tarehe 9 Februari 1974  huko Kindu. Baada ya ya shule  ya Msingi alingia


seminari ndogo ya Mama yetu wa Mitume huko Kindu (1987-1991), baadaye akaendelea na mafunzo ya malezi huko jimbo la  Kasongo (1991-1992). Tangu 1992 hadi 1995 mafunzo ya falsafa katika


seminari kuu ya Monsinyo  Cleire wa Kasongo na 1999 hadi 2000 Taalimungu seminari kuu ya Mtakatifu Pio X huko Murhesa Bukavu. Alipewa daraja la upadre tarehe 6 Januari 2002 kwa ajili ya


jimbo la Kindu. Baada ya upadrisho alijikita katika utume mbalimba wa parorokia na seminari, vituo vya caritas na mjumbe wa masuala ya uchumi wa jimbo 2003 hadi 2013. Aliendelea na  masomo


katika Chuo Kikuu cha Kipapa cha Gregoriana hadi  Udaktari katika Historia na Urithi wa Tamaduni wa Kanisa (2013-2020), wakati huo huo akiwa anatoa huduma yake ya kichungaji katika Jimbo la


Tivoli, kama kwenye parokia ya Mtakatifu Maria na Mtakatifu Mauro (2016-2020).