Sweden kuimarisha doria za mpakani

feature-image

Play all audios:

Loading...

Waziri Mkuu wa nchi hiyo, Ülf Kristensen, amewaambia waandishi wa habari kwamba uamuzi kuhusiana na suala hilo utatolewa Alhamis. Kristensen amesema kuwa wanaimarisha usalama wa Sweden kwa 


lengo la kuwazuia watu walio na mafungamano hafifu na Sweden, kuja kufanya uhalifu au kufanya vitendo vinavyokwenda kinyume na maslahi ya kiusalama ya Sweden. WANAUME WAWILI WA IRAK WACHOMA


QUR'AN MBELE YA BUNGE LA SWEDEN. Hapo jana, wanaume wawili raia wa Irak, Salwan Momika na Salwan Najem, walikichoma kitabu cha Qur'an mbele ya bunge la Sweden. Wawili hao awali


waliwahi kufanya vitendo hivyo nje ya msikiti mkuu wa Stockholm na mbele ya ubalozi wa Irak katika mji huo, vitendo vilivyolaaniwa pakubwa na kupelekea mivutano kati ya Sweden na mataifa ya


Kiislamu.